
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Taarifa ni kwamba nyota wa Arsenal Mesut Ozil raia wa Ujerumani anadalili kubwa za kutua Barcelona, Januari mwakani na tayari ada yake imetajwa kuwa ni Pauni 20 milioni.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 29, atamaliza mkataba wake katika klabu ya Arsenal Juni mwakani na uongozi wa klabu yake una wasiwasi kwamba wanaweza kumtoa bure kwa hiyo uweze kano wa kumuuza kwa kiasi hicho cha pesa ni mkubwa.
Katika siku za karibuni kocha wa Arsenal, Arsene Wenger alisema kuna dalili kubwa mchezaji huyo akarudi Hispania.
Mchezaji huyo alijiunga na Arsenal akitokea Real Madrid mwaka 2013 na amefunga mabao 24 na kutengeneza mabao 93 katika michezo 171 akiwa na kikosi cha Arsenal.
Habari ni kwamba Barcelona inataka kuongeza kiwango na wameshaanza kuongea na wakala wa Ozil, Dr ErkutSogut. Lakini imefahamika kuwa kuna klabu nyingine sita ambazo zinamwania mchezaji huyo katika dirisha la usajili la Januari.
Imefahamika kuwa mchezaji huyo atapewa mkataba ambao utamalizika 2020.
Barcelona kwa sasa ina nguvu katika La Liga ikiwa inashika nafasi ya kwanza kwa tofauti ya pointi nne baada ya kucheza mechi 12. Hata hivyo wanataka kuongeza moto katika kikosi
Post A Comment: