KLABU ya Azam FC, imemsajili mshambuliaji, Benard Athur kutoka klabu ya Liberty Professionals  ya nchini Chana.


Azam inadaiwa kumsajili mchezaji huyo kwa mkataba wa miaka miwili na amechukua nafasi ya aliyekuwa mshambuliaji wao, Mghana Yahya Mohamed aliyevunjiwa mkataba kwa makubaliano maalumu.

Hata hivyo, licha ya picha inayomwonyesha mchezaji huyo akikabiziwa jezi na Afisa Mtendaji Mkuu wa Azam,  Abdul Mohamed, Afisa habari wa klabu hiyo, Jaffar Idd Maganga hakutaka kuweka wazi na amesisitiza, taarifa kamili itatolewa kesho.

Huo ni usajili wa kwanza kwa Azam , waliofufanya katika dirisha dogo lililofunguliwa Novemba 15 na linatarajiwa kumalizika, Desemba 15.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: