
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Kocha Antonio Conte ameingia matatani kwa mara nyingine, baada ya kuibua mzozo na beki kisiki David Luiz.
Conte na Luiz walitoleana maneno makali kwenye mazoezi, Chelsea ilipokuwa ikijiandaa na mchezo wa Ligi Kuu England dhidi ya Manchester United.
Libero huyo wa kimataifa wa Brazil, juzi alikuwa jukwaani katika mchezo walioshinda bao 1-0 dhidi ya Man United kwenye Uwanja wa Stamgord Bridge.
Uamuzi wa kumuweka benchi Luiz umeanza kupigiwa kelele na wadau wa soka akiwemo mchambuzi maarufu Gary Neville.
Nahodha huyo wa zamani wa Manchester United, alisema Conte anaweza kufukuzwa kwa uamuzi mbaya wa kumuweka benchi Luiz.
Hii ni mara ya pili kwa kocha huyo kuibua mzozo na mchezaji wake, awali alimtenga Diego Costa kabla ya kumpiga bei Atletico Madrid.
"David ana ushawishi mkubwa ndani ya vyumba vya kuvalia nguo kama John Terry, endapo ataendelea kusugua benchi kwa wiki mbili au tatu huku kamera zikiendelea kumuonyesha jukwaani, Conte anaweza kufukuzwa,"alisema Neville.
Muda mfupi baada ya kuibuka mzozo huo, Conte alidai mchezaji huyo atasota benchi muda mrefu kwa madai ya utovu wa nidhamu.
Post A Comment: