ads

BAADHI ya wananchi na wafanyabiashara katika Manispaa ya Bukoba, wameelezea kushangazwa na uhaba wa sukari na kupanda bei kwa bidhaa hiyo ambayo kwa sasa inapatikana kwa Sh 2,500 hadi Sh 2,700 licha ya kuwepo kwa Kiwanda cha Sukari cha Kagera wilayani Missenyi mkoani Kagera.


Wananchi hao wamesema bei hiyo ya sukari ni kinyume cha bei elekezi ya Serikali ambayo iliagiza kilo moja ya sukari iuzwe kwa Sh 1,800.

Anitha John ni mfanyabiashara katika soko kuu la Bukoba anayeuza bidhaa mbalimbali ikiwemo sukari ambaye amesema sukari imepanda bei na ameamua kuacha kuuza kwa sababu kwa wakala kilo 50 zinauzwa Sh 100,000 na kwenye stakabadhi wanaandikiwa 90,000 na wakati wa nyuma kilo hizo 50 walinunua kwa Sh 76,000.

“Jambo la kushangaza si kwamba sukari haipo maana sukari inashushwa na kupelekwa kwenye maghala ukienda kwenye ghala kununua unaambiwa hakuna sukari, jambo ambalo ni tatizo kwa wafanyabiashara wadogo kama mimi, vinginevyo Serikali itoe vibali kwa kila mtu akajinunulie kiwandani ili biashara isikwame,” alieleza John.

Sebastiani Tweyambe ambaye ni mfanyabiashara mwingine wa bidhaa hiyo, alisema wiki mbili zilizopita sukari iliuzwa kwa Sh 2,000 wakati Rais John Magufuli alipotoa bei elekezi ya Sh 1,800, sasa baada ya bei kushuka inazidi kupanda mpaka sasa imefikia Sh 2,400 hadi 2,500 kutokana na wanavyonunua mzigo.
DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA

ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: