Dirisha dogo la usajili linafunguliwa wiki ijayo, huku viongozi wa timu wakianza kuwindana ili kudaka wachezaji nyota kwa ajili ya kuongeza makali kwenye vikosi vyao.


Simba inaongoza ikiwa na alama 19 sawa na Azam lakini wakiwa na faida ya uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa, wakati Yanga yenyewe ina pointi 17 kama za Mtibwa Sugar, ila uwiano wa mabao unawabeba mbele yao.

Yanga iliyolazimishwa sare mbili mfululizo katika mechi zao zilizopita ikiwa ile na watani zao Simba walifungana nao bao 1-1 kabla ya Singida United kuibana na kutoka nao suluhu, imeachwa pointi mbili na Simba katika msimamo wa ligi.

Kocha Lwandamina ameuambia uongozi kuwa, katika dirisha dogo anataka mastraika mawili tu wa kuimaliza Simba.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: