
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
KOCHA wa Simba, Jackson Mayanja amesema ushindi wa Yanga na Azam
hauwatishi na kwamba kikosi chake kitapambana mpaka dakika za mwisho.
Yanga na Azam zilimaliza mechi zao za viporo juzi, ambapo mabingwa
watetezi Yanga waliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Mgambo JKT na
Azam ilishinda mabao 2-0 dhidi ya Majimaji.
Akizungumza kwa njia ya mtandao kutoka Zanzibar ilipo
kambi ya Simba, Mayanja alisema bado timu yake ina nafasi nzuri kwenye
ubingwa kwani soka lolote linaweza kutokea.
Ushindi wa juzi umeifanya Yanga kufikisha pointi 62 kileleni mwa
msimamo wa ligi hiyo, Azam ikiwa nafasi ya pili kwa pointi 58 na Simba
iko nafasi ya tatu na pointi 57, timu zote zimebakiza mechi tano
kumaliza ligi.
βNajua ushindi wa Yanga na Azam katika mechi zake umetuweka kwenye
mazingira magumu kwa sababu wenzetu wameshinda mechi nyingi kutuzidi,
lakini bado hiyo siyo sababu ya sisi kukata tamaa, tutapambana mpaka
dakika ya mwisho,β alisema.
Simba kesho ina kibarua kigumu itakapomenyana na Azam kwenye Uwanja
wa Taifa Dar es Salaam. Mechi hiyo inatarajiwa kuwa ngumu na ya vuta
nikuvute kutokana na kila timu kuhitaji ushindi.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
Post A Comment: