ads

KOCHA wa Simba, Jackson Mayanja amesema ushindi wa Yanga na Azam hauwatishi na kwamba kikosi chake kitapambana mpaka dakika za mwisho.


Yanga na Azam zilimaliza mechi zao za viporo juzi, ambapo mabingwa watetezi Yanga waliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Mgambo JKT na Azam ilishinda mabao 2-0 dhidi ya Majimaji.

Akizungumza kwa njia ya mtandao kutoka Zanzibar ilipo kambi ya Simba, Mayanja alisema bado timu yake ina nafasi nzuri kwenye ubingwa kwani soka lolote linaweza kutokea.

Ushindi wa juzi umeifanya Yanga kufikisha pointi 62 kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo, Azam ikiwa nafasi ya pili kwa pointi 58 na Simba iko nafasi ya tatu na pointi 57, timu zote zimebakiza mechi tano kumaliza ligi.

“Najua ushindi wa Yanga na Azam katika mechi zake umetuweka kwenye mazingira magumu kwa sababu wenzetu wameshinda mechi nyingi kutuzidi, lakini bado hiyo siyo sababu ya sisi kukata tamaa, tutapambana mpaka dakika ya mwisho,” alisema.

Simba kesho ina kibarua kigumu itakapomenyana na Azam kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Mechi hiyo inatarajiwa kuwa ngumu na ya vuta nikuvute kutokana na kila timu kuhitaji ushindi.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA

ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: