Kiungo Eden Hazard amekiri kuwa kucheza chini ya kocha wa Real Madrid, Zinedine Zidane ndiyo lengo lake katika siku za usoni.


Winga huyo wa Chelsea amekuwa akihusishwa na kutaka kuhamia Santiago Bernabeu kila wakati, tangu akiwa na Lille.

Japokuwa kwa sasa hafikiri kuhusu uhamisho huo, lakini Hazard amekiri kuwa ndoto yake kucheza chini ya mtu anayemvutia zaidi tangu utoto wake.

"Kila mtu anajua heshima niliyokuwa nayo kwa Zidane kama mchezaji, pia kama kocha ni mtu ninayemvutia," aliimbia RTL.

"Sijui nini kitatokea katika maisha yangu ya soka ya baadaye, lakini itakuwa ni ndoto yangu kucheza chini ya Zidane.

"Lakini kwa sasa nafurahi maisha yangu Chelsea. Bado kuna mambo natakiwa kupata nikiwa hapa akili yangu yote ipo kama mchezaji wa Chelsea."
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: