Mshambuliaji wa Chelsea, Alvaro Morata amewatoa hofu mashabiki na uongozi wa klabu hiyo kwamba ataendelea kuitumikia klabu hiyo hata baada ya mkataba wake kumalizika.


Morata amelazimika kutoa ufafanuzi huo baada ya kueleza kwenye mahojiano na Gazeti la Dello Sport kuhusu kuondoka England baada ya mkataba wake kumalizika.

Alisisitiza kwamba nia yake ni kuitumikia Chelsea kwa miaka 10 baadaye, jambo ambalo limeondoa hofu kwa mashabiki  kwamba mchezaji huyo angetimka London baada ya mkataba wake kumalizikika.

Pia alisisitiza kwamba anafurahia maisha ya kucheza soka Stamford Bridge ambako amesajiliwa kuihudumia timu hiyo kwa mkataba wa miaka mitano alipowasili Juni mwaka huu akitokea Real Madrid.

Aliongeza kuwa Jambo la msingi kwake ni kuwa katika kiwango kizuri wakati wote na kuimarika zaidi.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: