
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania aliyesajiliwa na klabu ya Polokwane City inayoshiriki Ligi Kuu ya nchini Afrika Kusini, Elias Maguli, amewataka wachezaji wengine wachangamkie fursa ya kucheza soka la kulipwa.
Maguli aliyewahi kucheza katika timu za Simba, Stand United na Ruvu Shooting, amesaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia Polokwane City baada ya kuachana na klabu ya Dhofar ya nchini Oman.
Akizungumza na gazeti la BINGWA jana, Maguli alisema hapa nchini kuna wachezaji wengi wenye uwezo wa kucheza soka la kulipwa lakini wanashindwa kuchangamkia fursa hiyo.
Aliwataja baadhi ya wachezaji ambao viwango vyao vinawaruhusu kucheza soka la kulipwa kuwa ni Jonas Mkude, Hassan Dilunga, Mohamed Hussein ‘Tshabalala’, Rafael Daudi, Mzamiru Yassin na Rajab Zahir.
Alisema wachezaji hao wanatakiwa kupambana na kuikabili changamoto ya kukatishwa tamaa ili kufikia malengo yao, viwango walivyonavyo havina tofauti na wale anaokutana nao katika klabu za nje.
“Tanzania kuna wachezaji wengi ambao wana uwezo wa kucheza soka la kulipwa, kinachowakwamisha ni kudharauliana wenyewe kwa wenyewe na kukatishana tamaa,” alisema Maguli.
Tetesi za awali zilidai kuwa straika huyo alikuwa na mpango wa kurejea kwenye klabu yake ya zamani ya Simba pamoja na Yanga katika dirisha dogo la usajili, lakini mambo yakaenda tofauti.
Post A Comment: