Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki Joshua Nassari, amekata rufaa kupinga hatua ya kuenguliwa wagombea wake wawili waliopitishwa kugombea udiwani kwenye uchaguzi mdogo wa marudio unaofanyika katika kata tano katika Jimbo la Arumeru Mashariki.


Akizungumza na waandishi wa habari, Nassari amesema kuwa amesikitishwa na uamuzi uliofanywa na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi huo kwani hawakuzingatia kanuni, taratibu na sheria za uchaguzi.

Nasari amesema amekata rufaa Tume ya Uchaguzi kupitia Mkurugenzi wa Taifa wa Uchaguzi kufikisha malalamiko yao kwani kutenguliwa kwa wagombea wao kutokana na kutofuatwa taratibu ikiwemo msimamizi wa uchaguzi msaidi kuwatengua wagombea wakati hana sifa ya kufanya hivyo.


ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: