
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
RAIS wa Shirikisho la soka la Italia, Carlo Tavecchio amethibitisha kwamba kocha wa Chelsea, Antonio Conte ana nafasi kubwa ya kuwa kocha wa kikosi cha Azzurri.
Timu ya soka ya taifa ya Italia kwa sasa haina kocha baada ya Gian Piero Ventura kufutwa kazi hivi karibuni kufutia timu hiyo kushindwa kufuzu fainali za Kombe la Dunia 2018 zitakazofanyika Russia.
Italia imeshindwa kufuzu fainali hizo kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 60 baada ya kutolewa na Sweden kwenye mechi za mchujo.
Mara ya mwisho Italia kushindwa kukamata tiketi ya fainali za Kombe la Dunia ilikuwa mwaka 1958, zilizofanyika Sweden. Mipango ya Italia kwenye michuano mikubwa kwa sasa ni kusubiri mikikimikiki ya Euro 2020.
Post A Comment: