RAIS wa Shirikisho la soka la Italia, Carlo Tavecchio amethibitisha kwamba kocha wa Chelsea, Antonio Conte ana nafasi kubwa ya kuwa kocha wa kikosi cha Azzurri.


Timu ya soka ya taifa ya Italia kwa sasa haina kocha baada ya Gian Piero Ventura kufutwa kazi hivi karibuni kufutia timu hiyo kushindwa kufuzu fainali za Kombe la Dunia 2018 zitakazofanyika Russia.

Italia imeshindwa kufuzu fainali hizo kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 60 baada ya kutolewa na Sweden kwenye mechi za mchujo.

Mara ya mwisho Italia kushindwa kukamata tiketi ya fainali za Kombe la Dunia ilikuwa mwaka 1958, zilizofanyika Sweden. Mipango ya Italia kwenye michuano mikubwa kwa sasa ni kusubiri mikikimikiki ya Euro 2020.

     
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: