
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
KOCHA wa Azam FC, Zeben Hernandez amechekelea ratiba ya Kombe la
Shirikisho barani Afrika na kudai kikosi chake kitafika mbali kwenye
michuano hiyo.
Kauli ya Zeben imekuja baada ya kuona ratiba hiyo ambayo mashindano
yake yanatarajia kuanza mwakani, na timu yake itaanza hatua ya kwanza
kwa kucheza na mshindi wa jumla wa mechi ya raundi ya awali kati ya
Orapa United ya Botswana na Mbabane Swallows ya Swaziland.
Zeben alisema Azam FC wamejiwekea malengo
ya kuingia hatua ya makundi ya michuano hiyo kutokana na usajili
uliofanywa.
“Tumefurahi namna ratiba ilivyopangwa, tumeanzia raundi ya kwanza
kutokana na ubora wa Azam FC tofauti na timu nyingine zinazoanzia raundi
ya awali, kifupi tumepanga kufika hatua ya makundi, namna gani
tutafikia ni kutokana na wachezaji waliosajiliwa kwani wana uzoefu,”
alisema.
Zeben alisema ili kufika hatua ya makundi lazima kazi kubwa ifanyike
na kila mtu kujituma kwenye nafasi yake na watajitahidi kujipanga kwa
ajili ya mechi za michuano hiyo ikiwemo kuwafanyia tathmini wapinzani
wao ambao wanatarajia kucheza naye.
“Naamini ni muda mzuri wa kujipanga zaidi kwani ni mashindano makubwa
kinachotakiwa ni sisi kuingia tukiwa tayari ili ushiriki wetu uwe mzuri
na kufika nafasi za juu zaidi,” alisema.
Azam FC itaanza kucheza ugenini na moja wa mshindi wa jumla wa mechi
ya raundi ya awali kati ya Orapa United ya Botswana na Mbabane Swallows
ya Swaziland Machi 10 hadi 12 mwakani kabla ya kurejeana nyumbani Azam
Complex kati ya Machi 17 na 19.
Endapo watafuzu, wataingia raundi ya mwisho ya mtoano watakayocheza
na moja ya timu 16 zilizotolewa kwenye raundi ya kwanza ya Ligi ya
Mabingwa Afrika, ikivuka itaingia moja kwa moja kwenye hatua ya makundi.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: