
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
NG’OMBE 185 wamekufa kwa kipindi cha kuanzia Oktoba hadi Desemba
mwaka huu katika ranchi ya Ruvu, mkoani Pwani kutokana na ukame.
Hayo yalisemwa na Meneja wa ranchi hiyo, Dk James Mtae wakati akitoa
maelezo kwa Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dk Charles
Tizeba wakati alipofanya ziara katika eneo hilo kwa ajili ya kubaini
changamoto mbalimbali zinazoikabili.
Akizungumzia ukame, Dk Mtae alisema mifugo hiyo ilikufa kutokana na
kukosa majani katika eneo hilo. Alisema hata yale yaliyoletwa kutoka
Kongwa mkoani Dodoma nayo yaliisha, hali iliyosababisha kuanza
kudhoofika na hatimaye kufa.
“Njaa haiji kwa haraka, ni jambo ambalo huanza kidogokidogo lakini
zipo jitihada mbalimbali ambazo zimefanywa katika kuokoa hali hiyo
kutokea,” alisema Dk Mtae wakati akijibu kwa nini alisubiri hadi mifugo
hiyo inadondoka bila kutafuta namna ya kuweza kuiokoa.
Alisema amejitahidi kwa kiwango cha kutosha, kwani ameweza kuisimamia
mifugo hiyo kwa namna mbalimbali ili iweze kuishi, lakini kwa bahati
mbaya na mabadiliko ya hali ya hewa, yaliyoleta ukame, ndio
yaliyosababisha maafa hayo.
Hata hivyo, Waziri Tizeba alisema licha ya kuwepo kwa jitihada
mbalimbali zilizofanyika, lakini kuna uzembe uliosababisha hali hiyo
kutokea.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: