
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
WATANZANIA wametakiwa kutoa taarifa
wanabaini uwepo wa mchele usioeleweka, baada ya kuibuka kwa taarifa ya mchele
bandia wa plastiki kukamatwa Nigeria.
Msemaji wa Mamlaka ya Chakula na Dawa
(TFDA), Gaudencia Simwanza alisema hayo jana .
Alisema wao sasa wana mifumo mizuri ya
kudhibiti uingizwaji wa bidhaa zisizofaa na mpaka sasa mfumo huo haujabaini
mchele wa aina hiyo nchini.
"Tunadhibiti na tuko makini
kufuatilia wafanyabiashara wanaoingiza vitu haramu na kama huo mchele ungekuwa
umeingia, tungeshajua," alisema.
Mwandishi wa habari hii alipomwuliza
ikitokea umeingizwa kimagendo nchini, Watamzania watautambua vipi, Gaudencia
aliwataka kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa watakapoona mchele wasiouelewa.
Mchele huo bandia ulikamatwa na Mamlaka
ya Mji wa Lagos, Nigeria wiki hii, ambapo walikamata magunia 102.
Taarifa kutoka nchini humo, zilieleza
kuwa uliingizwa nchini humo na wafanyabiashara haramu na unafanana na mchele wa
kawaida, hivyo ni ngumu kuutofautisha na mchele wa kawaida.
Kutokana na kusambaa kwa kasi kwa mchele
huo, huwezi kuutambua kwa haraka hadi pale unapopikwa ndipo unaweza kuona ni
mchele wa plastiki. Hata hivyo baadhi ya wataalamu walisema kabla ya kuupika
mchele huo ukilowekwa kwenye chombo chenye maji unaelea tofauti na halisi ambao
huzama.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: