
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania, Dkt. John Magufuli na mke wake
Mama Janeth Magufuli leo wameshiriki Misa ya Krismasi katika Kanisa Kuu
la Moyo Mtakatifu wa Yesu mkoani Singida.
Rais amewahi kusali katika kanisa hilo kabla ya uchaguzi mkuu mwaka
jana huku akimkumbuka Sister mmoja aliyemkabidhi rozali na kumuahidi
kushinda nafasi ya urais katika uchaguzi huo.
Akizungumza katika ibada hiyo Rais Magufuli amesema rozali
hiyo alikuwa anazunguka nayo kwenye ziara zake za kampeni hadi mwisho na
kufanikiwa kupata kura za kutosha zilizompa ushindi.
Amesema kusali hapo ni moja ya sababu kubwa ya siri ya ushindi wake,
na hivyo kuungana na wakazi wa mkoa wa Singida na watanzania wote
kusherehekea kuzaliwa kwa Yesu Kristo.
Magufuli ametumia fursa hiyo kuwataka watanzania kutumia Sikukuu ya
Krisimasi kuimarisha upendo, kuvumiliana na kutobaguana, kwani njia ya
upendo itasaidia taifa kujipatia maendeleo.
Aidha, amewataka wakulima kuhakikisha wanazitumia vizuri mvua za sasa
katika kuchapa kazi ya kilimo kwa nguvu zote pamoja na kulima mazao
yanayostahimili ukame.
Amesema Sikukuu ya Krismasi kunadhihirisha kauli mbiu ya 'hapa kazi
tu', kwani Yesu Kristo alikuwa fundi mzuri wa useremala hivyo kuwataka
watanzania kumuiga, na pia akiwataka wakazi wa mkoa wa Singida, kuongeza
uzalishaji wa zao la alzeti ili kuviwezesha viwanda vya kukamua mafuta
ya alzeti kupata mbegu nyingi.
Awali Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Singida, Edward Mapunda,
amewakumbusha wakazi wa mkoa huo kuhakikisha wanatunza mazingira ili
yaweze kuwatunza na kuwaepusha na ukame wa mvua.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: