MAKAMU wa Rais, Samia Suluhu Hassan amewataka wazazi na walezi wa visiwani Zanzibar, kuacha tabia ya kuwaoza wasichana wakiwa na umri mdogo, bali wawasomeshe kwa ajili ya manufaa yao ya jamii kwa ujumla.


Samia alisema hayo kwa nyakati tofauti, wakati akizindua madarasa ya kisasa iliyojengwa kwenye eneo la Kilimani na kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa na ujenzi wa msikiti mkubwa kuliko yote nchini Tanzania unaojengwa katika eneo la Ijitimai Kidoti mkoani Kaskazini Unguja.

Ujenzi huo unafanywa kwa michango ya wananchi. Alisema hayo katika siku yake ya kwanza ya ziara ya Kikazi Unguja.

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Makamu wa Rais, Zanzibar, ilieleza kuwa makamu huyo wa Rais yupo katika ziara visiwani Zanzibar.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Samia alisema kama wazazi na walezi watasomesha watoto wa kike, elimu watakayopata itasaidia kwa kiasi kikubwa wasichana hao, kufanya maamuzi sahihi na yenye tija katika jamii.

Alisisitiza kuwa elimu ni haki ya msingi kwa mtoto wa kike, hivyo ni muhimu kwa jamii ya Zanzibar ihakikishe watoto wa kike wote wanapata elimu, kwani watakuwa na uwezo wa kuchagua na kuandaa mustakbali wa maisha yao ya baadaye, ikilinganishwa na hali ilivyo sasa kwenye baadhi ya maeneo.

Kuhusu elimu ya dini, aliwahimiza wazazi na walezi, kuwalea watoto katika maadili mema kwa kuzingatia maandiko matakatifu ya Mtume Mohammad (S.A.W).

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: