RAIS mstaafu wa awamu ya pili, Ally Hassan Mwinyi na Rais mstaafu wa Zanzibar, Dk. Salmin Amour Juma, ni miongoni mwa vigogo wanaotajwa kuwamo katika orodha ya zaidi ya wakazi 10,000 wanaotakiwa kuhama kwenye vijiji vinne vilivyoko Mkuranga mkoani Pwani kabla hawajaondolewa kwa nguvu.


Mbali na Mwinyi, maarufu kama Mzee Ruksa na Dk. Salmin “Komandoo”, wengine wanaotajwa kuwamo katika orodha hiyo, ni Waziri Mkuu wa zamani aliyewahi pia kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU sasa Umoja wa Afrika) , Dk. Salim Ahmed Salim; Mbunge wa Jimbo la Mkuranga na Katibu wa Wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdallah Ulega, na aliyekuwa Naibu Waziri wa Fedha katika serikali ya awamu ya nne, Adam Malima.

Wengine ni Dk. Ramadhani Dau, mmoja wa watoto (anayedaiwa wa kike mkubwa) wa Waziri Mkuu wa zamani katika Serikali ya awamu ya kwanza, Rashidi Kawawa na majaji wastaafu.

Vigogo hao, pamoja na wakazi wa vijiji vinne vya Kata ya Mwanambaya, wanatakiwa kuondoka ndani ya siku 21 ili kupisha eneo hilo kuingizwa katika mpango wa upimaji wa mji.

Taarifa zilizotolewa katikati ya wiki kwenye katika mkutano uliofanyika katika kijiji cha Mwanambaya na kuhusisha wananchi wa vijiji vyote vinne, zilieleza kuwa wakazi hao wanatakiwa kuondoka kuanzia Desemba 20, 2016, ambayo ni siku iliyotolewa notisi ya kutakiwa wafanye hivyo.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: