
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
RAIS mstaafu wa awamu ya pili, Ally Hassan
Mwinyi na Rais mstaafu wa Zanzibar, Dk. Salmin Amour Juma, ni miongoni
mwa vigogo wanaotajwa kuwamo katika orodha ya zaidi ya wakazi 10,000
wanaotakiwa kuhama kwenye vijiji vinne vilivyoko Mkuranga mkoani Pwani
kabla hawajaondolewa kwa nguvu.
Mbali na Mwinyi, maarufu kama Mzee Ruksa na Dk. Salmin “Komandoo”,
wengine wanaotajwa kuwamo katika orodha hiyo, ni Waziri Mkuu wa zamani
aliyewahi pia kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU sasa
Umoja wa Afrika) , Dk. Salim Ahmed Salim; Mbunge wa Jimbo la Mkuranga
na Katibu wa Wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdallah Ulega, na
aliyekuwa Naibu Waziri wa Fedha katika serikali ya awamu ya nne, Adam
Malima.
Wengine ni Dk. Ramadhani Dau, mmoja wa watoto (anayedaiwa wa kike
mkubwa) wa Waziri Mkuu wa zamani katika Serikali ya awamu ya kwanza,
Rashidi Kawawa na majaji wastaafu.
Vigogo hao, pamoja na wakazi wa vijiji vinne vya Kata ya Mwanambaya,
wanatakiwa kuondoka ndani ya siku 21 ili kupisha eneo hilo kuingizwa
katika mpango wa upimaji wa mji.
Taarifa zilizotolewa katikati ya wiki kwenye katika mkutano
uliofanyika katika kijiji cha Mwanambaya na kuhusisha wananchi wa vijiji
vyote vinne, zilieleza kuwa wakazi hao wanatakiwa kuondoka kuanzia
Desemba 20, 2016, ambayo ni siku iliyotolewa notisi ya kutakiwa wafanye
hivyo.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: