
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
MBUNGE wa Jimbo la Ubungo, Saed Kubenea, ameahidi kupambana na ubadhirifu utakaojitokeza ndani ya jimbo lake.
Mbunge huyo pia amesema hayupo tayari kumvumilia mtendaji
anayesababisha kero kwa wananchi badala ya kufanya jitihada ya
kuzitatua.
Alitoa kauli hiyo juzi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kata ya Kimara, Mtaa wa Mavurunza wilayani Ubungo.
Kubenea alisisitiza kuwa utendaji mbovu ni chanzo cha kuzorotesha maendeleo ndani ya jimbo.
Alisema kuwa lengo lao ni kuwapatia wananchi huduma muhimu ambazo ni
haki yao kuzipata kama maji, barabara, shule, huduma za afya, soko na
vituo vya polisi.
“Tutapambana na ufisadi na ubadhirifu wa namna yoyote utakaogundulika
kufanywa na viongozi ndani ya eneo letu, sisi tumedhamiria kuleta
mabadiliko na maendeleo kwa wananchi tunaowaongoza, hivyo hatupo tayari
kumuacha mtu aharibu taswira yetu,” alisisitiza.
Mbunge huyo kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(Chadema), alisema kama kuna tatizo ndani ya uongozi kwenye kata,
litatuliwa kwa njia ya vikao husika, hawataruhusu watu kuondoka
madarakani bila kufuata utaratibu.
Kubenea alisema tayari hatua za awali zimeanza kuchukuliwa kutatua
suala la ukosefu wa maji, shule na barabara ikiwamo mazungumzo kuhusu
ujenzi wa dharura wa shule ya sekondari ndani ya siku 90 ili kusajili
wanafunzi wenye uwezo ambao walikosa nafasi ya kuendelea na masomo.
“Watoto 859 wamefaulu kujiunga na masomo ya sekondari, lakini 492 tu
ndiyo wamepangiwa shule…kwa sasa tunahitaji madarasa manane ili
kuwezesha idadi hiyo ya wanafunzi kuanza masomo,” alisema.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: