
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
KOCHA wa Yanga, Mzambia George Lwandamina
amepingana na maoni kwamba Yanga imepangwa na vibonde katika Raundi ya
Awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika mwakani.
Mabingwa wa Tanzania, Yanga wataanza na Ngaya de Mbe ya Comoro na
Lwandamina amesema hiyo si timu ya kubeza kwa kuwa ratiba nzima ya
raundi ya awali imehusisha timu zenye viwango sawa.
“Droo iko sawa, wapinzani wetu si timu ya kubeza natarajia ushindani
na tutahitaji maandalizi mazuri kabla ya mchezo huo,”alisema.
Yanga wataanzia ugenini wikiendi ya Februari 10 hadi 12 kabla ya
marudiano wikiendi ya Februari 17 hadi 19, mwaka huu na wakivuka hatua
hiyo watakutana na mshindi kati ya Zanaco ya Zambia na APR ya Rwanda
katika Raundi ya kwanza wakianzia nyumbani Machi 10 hadi 12 kabla ya
marudiano Machi 17 hadi 19 mwakani, 2017.
Lakini Lwandamina amesema hawezi kuzungumzia hatua inayofuata
kukutana na mshindi kati ya Zanaco na APR kabla ya kuvuka mtihani uliopo
mbele yake dhidi ya mabingwa Comoro.
“Siwezi kuzungumzia mechi hiyo, subiri wakati wake utakapofika ndipo
nitaizungumzia kwa sasa tunaelekeza nguvu zetu kwenye mtihani uliopo
mbele yetu,”alisema.
Lwandamina aliyejiunga na Yanga mapema Novemba, anakabiliwa na
changamoto ya kuipiku rekodi ya mtangulizi wake, Mholanzi Hans van der
Pluijm ambaye mwaka huu aliifikisha Yanga hatua ya 16 Bora ya Ligi ya
Mabingwa Afrika na kutulewa na Al Ahly ya Misri.
Yanga ikaangukia kwenye kapu la kuwania hatua ya makundi ya Kombe la
Shirikisho, ambako ilifanikiwa kuitoa Sagrada Esperanca ya Angola na
kuingia Kundi A pamoja na TP Mazembe ya DRC, MO Bejaia ya Algeria na
Medeama SC ya Ghana.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: