WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amewataka wadau wa elimu mkoa wa Mbeya kujitafakari baada ya Mkoa huo kufanya vibaya katika matokeo ya mtihani wa darasa saba mwaka huu.


Profesa Ndalichako ametoa agizo hilo kwenye Mahafali ya Pili ya Mafunzo ya Uongozi na Usimamizi Elimu ya Chuo cha Wakala wa Maendeleo ya Utawala wa Elimu(ADEM) yaliyofanyika jijini Mbeya.

Amesema  mkoa wa Mbeya umekuwa wa 22 kati ya mikoa 26 hivyo kudhihirisha kuwa ulifanya vibaya na ni lazima kila mdau ajitafakari ni kwa namna gani amechangia matokeo hayo mabaya.

Ameagiza uongozi ngazi ya mkoa na halmashauri kuhakikisha unajipanga kutumia fursa zilizopo ili kuondokana na aibu kwa kufanya vizuri kwenye mitihani ya kitaifa.

Amewataka pia walimu wakuu kuhakikisha wanakuwa wasimamizi wa kwanza wa raslimali za shule sambamba na kusimamia viwango bora vya taaluma.

Wahitimu wa mafunzo hayo ya mwaka mmoja ambao wote ni walimu wakuu kutoka shule za mikoa ya Mbeya, Songwe, Njombe na Iringa, waliiomba Serikali kuendeleza kozi hiyo wakisema imewajengea uwezo zaidi wa kiutawala.

Mwalimu Josephat Mahimbi akisoma risala alisema, awali walimu wakuu walikuwa na wakati mgumu kiutendaji kwa kuwa walikuwa wakiteuliwa kushika nyadhifa hizo pasipo kuwa na muongozo wowote.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: