
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
SIKU chache baada ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter
Muhongo kueleza kiu ya serikali ya kuona nchi inaondokana na mgawo wa
umeme, kudhibiti kukatikakatika kwa umeme, kuzalisha umeme wa uhakika na
unaotabirika kwa maendeleo ya viwanda, lakini pia kuwa na umeme nafuu,
Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) limekuja na majibu ya hoja hizo,
huku likisisitiza kuwa umeme utapanda kwa wateja wa kati na si wa chini.
Majibu hayo yalitolewa juzi usiku kwenye kipindi cha Kipima Joto
kinachorushwa hewani na Kituo cha televisheni cha ITV na Mkurugenzi
Mtendaji wa Tanesco Felchesmi Mramba, huku akishuhudiwa na Mkurugenzi
Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA), Felix
Ngamlagosi, aliyetoa pia ufafanuzi wa masuala kadhaa.
Hatua hiyo imekuja ikiwa ni wiki moja kupita tangu Ewura ilipopokea
maombi kutoka Tanesco ya kutaka kuongeza bei ya umeme kwa wastani wa
asilimia 18.19 kwa mwaka 2017.
Katika maelezo yake ya juzi usiku, Mramba alisema kutokana na shirika
hilo kuwajali wateja wa kipato cha chini, wateja hao hawataathirika na
mapendekezo ya bei mpya, na badala yake watabakia na bei iliyopo sasa.
Mkurugenzi huyo pia alisisitiza kuwa shirika hilo halina mpango wa
kurudisha tozo ya kuunganishiwa umeme ya Sh 5,000 na gharama ya huduma
kwa kila mwezi ya Sh 5,520 ambazo ziliondolewa mwezi Aprili mwaka huu.
Mapendekezo ya kupandisha bei ya umeme
Akifafanua mapendekezo hayo, Mramba alisema bei za umeme
zinazotumika, zinatakiwa kutumika hadi Desemba 31, mwaka huu na baada ya
hapo Januari mwakani sheria inataka bei mpya zitolewe. Alisema pamoja
na mapendekezo hayo, walichoomba ni kuongezeka kwa bei kidogo ambayo
haiwezi kuwaumiza wananchi, bali itaboresha zaidi huduma na kufanya
wazipate kwa uhakika kama alivyoagiza Waziri Muhongo.
“Tanesco ilitakiwa kufanya tathmini ya gharama za uzalishaji,
usafirishaji na usambazaji umeme na kupeleka mapendekezo hayo Ewura, ili
kupitiwa na wadau, sasa suala la kupanda au kushuka kwa bei itategemea
na mapitio ya tathmini ya gharama za kuzalisha, kusafirisha na kusambaza
tulizowasilisha Ewura,” alisema Mramba.
Akizungumzia kuhusu kuondolewa kwa tozo ya gharama za kila mwezi
pamoja na tozo ya kuunganishiwa umeme kwa wateja wapya, Mramba alisema
katika mapendekezo hayo tozo hizo hazipo na wala hawana mpango wa
kuzirudisha na kwamba wateja wa chini wao wataendelea kununua umeme kwa
bei iliyopo sasa.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: