Jeshi la Polisi mkoani Mtwara limeuzuia mkutano wa uliotarajiwa kuhutubiwa leo na Katibu Mkuu wa CUF, Seif Sharif Hamad.


Mkutano huo ulitegemewa kuanza saa 5 asubuhi lakini askari walionekana wakizunguka geti la kuingia chuo cha Stella Maris (Stemmuco) ambako CUF walitegemea kutumia ukumbi wao.

Katika eneo la chuo hicho yalionekana magari matatu ya askari ambayo pia yalikuwa yakizunguka katika mji wa Mtwara na gari moja la maji ya kuwasha likiwa limesimama kando ya eneo la chuo hicho.

Mkurugenzi wa habari, uenezi na uhusiano wa Umma CUF, Mbarala Maharagande amesema mkutano huo ulilenga kukagua shughuli za chama, kupata maoni ya wanachama pamoja na mapendekezo ya namna ya kuboresha utendaji wa chama kwa ngazi za chini.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: