
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Mkoani Dodoma, mtu anayehusishwa na vitendo vya ugaidi, Azan
Abubakary amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Dodoma Mjini na
kusomewa mashtaka yake.
Akiwa amevalia fulana ya rangi ya bluu na kijani na suruali nyeusi na
viatu vya matairi (maarufu kama katambuga), alisomewa shtaka lake mbele
ya Hakimu Mwajuma Lukindo.
Mshtakiwa huyo anashtakiwa kwa makosa ya kufadhili ugaidi chini ya
kifungu cha 13 cha sheria ya makosa ya kuzuia ugaidi namba 21 ya mwaka
2002. Ilidaiwa kuwa Mei 15, 2016 alimtumia fedha Mohamed Ibrahim kwa
njia ya M-Pesa kiasi cha Sh 265,000 katika namba +254 708104109 kwa
ajili ya kufanyia ugaidi nchini.
Aidha Julai 22, 2016 Abubakary alionekana eneo la Dodoma akituma
fedha kwa njia ya M-Pesa kwa Mohamed Ibrahim Sh 148,000 kwa ajili ya
kufanya vitendo vya ugaidi. Hakimu Lukindo alisema mshtakiwa hatakiwi
kujibu chochote kwa sababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza
shauri hilo.
Wakati huo huo, Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma katika taarifa yake
kwa vyombo vya habari imesema kwamba mtuhumiwa huyo aliyefikishwa
mahakamani ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) Kitivo cha Afya
na yupo mwaka wa pili.
Taarifa hiyo iliyosainiwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma,
Lazaro Mambosasa, mtuhumiwa alikamatwa Nzega mkoa wa Tabora baada ya
kugundulika kuwa anajihusisha na mtandao wa ugaidi wa kundi la ‘Al
Shabaab’ kutoka Somalia.
Kamanda alisema mtuhumiwa alikamatwa kutokana na taarifa za
Intelijensia ya Polisi katika masuala ya ugaidi. Katika tukio lingine,
polisi wanafanya uchunguzi wa kifo cha mashaka kilichotokea Novemba 15,
mwaka huu saa 12 jioni katika Hoteli ya Kitemba katikati ya mji wa
Dodoma.
Katika tukio hilo, Ofisa mstaafu wa Magereza aliyefahamika kwa jina
la DCP – Luvugo Chiza, mwenye miaka 62, mkazi wa Kigoma aliyekuwa
akitokea Dar es Salaam kwenda Kigoma, alishuka Dodoma na kulala katika
hoteli hiyo kwa ajili ya kushughulikia viwanja vyake CDA.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: