MWENYEKITI wa Bodi ya Taifa ya Parole, Augustino Mrema amemwomba Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kuliamuru Jeshi la Magereza liruhusu kupunguza msongamano wa wafungwa katika magereza kwa mujibu wa sheria za nchi, pamoja na kuachia wafungwa waliolipiwa faini.


Aidha, ametaka viongozi wa Magereza au wa serikali waliokwamisha wafungwa waliotimiza masharti yote wasiachiliwe kwa makusudi, wachukuliwe hatua za kinidhamu.

Aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Idara ya Habari – Maelezo, jijini Dar es Salaam ambako alitoa kilio chake dhidi ya Magereza kwamba wanakwamisha kazi ya kupunguza msongamano wa wafungwa.

Katika barua aliyoiandika kwenda kwa Waziri Mkuu, ameeleza kuwa Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dodoma alisema kwa sasa magereza yaliyopo katika mkoa huo kuna wafungwa 30 ambao mchakato wake umekwama kukamilika kutokana na ukosefu wa fedha.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: