
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam imetoa amri ya
kusimamisha kesi ya wizi wa Sh bilioni 3.9 katika Akaunti ya Madeni ya
Nje (EPA) inayomkabili mfanyabiashara maarufu, Jayantkumar Patel,
maarufu kwa jina la “Jeetu Patel” na wenzake watatu.
Jopo la mahakimu watatu likiongozwa na Hakimu Ignas Kitusi lilitoa
amri ya kusimamisha kesi hiyo jana, hadi kesi yao ya kikatiba
iliyofunguliwa katika Mahakama Kuu itakapotolewa uamuzi.
Hatua hiyo inatokana na maombi yaliyowasilishwa ya kusimamishwa kwa
kesi hiyo yaliyowasilishwa na mawakili wa upande wa utetezi, Martin
Matunda na Mabere Marando wakidai mshitakiwa alifungua kesi Mahakama Kuu
akidai kuvunjiwa haki ya kikatiba na Mwenyekiti Mtendaji wa kampuni ya
IPP, Reginald Mengi.
Katika kesi hiyo, inadaiwa kuwa, Aprili 23, mwaka jana, Mengi
alitumia vyombo vya habari kumhukumu Jeetu kwa kumuita ‘Fisadi Papa’
kabla Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu inayosikiliza kesi dhidi ya mteja
wao haijatoa hukumu.
Mawakili hao wanadai wamefungua kesi hiyo wakiomba tafsiri ya kisheria kwa kuwa wanaamini haki ya mteja wake imevunjwa.
Mbali na Mengi, Jeetu amefungua kesi hiyo dhidi ya Mwanasheria Mkuu
wa Serikali, na Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) ambao anadai kwa nafasi
zao walishindwa kutimiza wajibu wao baada ya Mengi kumhukumu kupitia
vyombo vya habari.
Katika kesi nyingine, mshitakiwa huyo amekata rufaa kupinga uamuzi wa
Mahakama Kuu ilioamuru majalada ya kesi zinazomkabili na wenzake,
kurudi Mahakama ya Kisutu ili ziendelee.
Jeetu pamoja na Devendra Patel, Amit Nady na Ketan Chohan
wanakabiliwa na kesi nne za wizi wa fedha kutoka kwenye Akaunti ya EPA
katika Mahakama ya Kisutu, zili funguliwa Novemba mwaka juzi.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: