
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Tabasamu
la kila mmoja kati yetu hutegemea usafi wa kinywa chake unaotokana na
kupiga mswaki na kusugua kwa umakini. Changamoto iliyopo ni namna ya
kufanya hivyo kwa ufasaha.
Wengi
hawafahamu njia sahihi za kupiga mswaki kwa ajili ya afya ya kudumu ya
kinywa inayoaanza hapo. Kinywa safi ni msingi wa afya njema ya mwili.
Afya
ya kinywa inaanza na meno yaliyo safi. Hili hufanyika kwa kutunza
maeneo na meno yanakutana na fizi katika hali ya usafi huzuia magonjwa
ya fizi na kuzuia kutoboka kwa meno.
Kufanikisha
usafi wa kinywa na meno, kila mmoja anapaswa kuzingatia upigaji sahihi
wa mswaki kila siku au inapohitajika. Yapo mambo mengi ya kuzingatia
wakati wa kupiga mswaki lakini nitaeleza matano kwa leo.
Kwa
afya njema ya kinywa chako, unashauriwa kupiga mswaki mara mbili kwa
siku. Wakati unafanya hivyo, usiwe na haraka. Chukua muda wa kutosha
kusugua meno yako yote kwa ukamilifu huku ukihakikisha kila kinachopaswa
kuondolewa kimefikiwa.
Kulingana
na umri, mazingira au hali ya afya, unashauriwa kutumia mswaki sahihi
utakaokufaa pamoja na dawa ya meno iliyo na madini ya floridi. Mswaki
mzuri ni ule ambao visafishio vyake havikuumizi na unaokaa vizuri
kinywani.
Watoto
wapewe mswaki unaofanana na umri wao ili kufanikisha hili. Wale wadogo
wasimamiwe ili kuzingatia namna ya upigaji na kuepuka kutomeza dawa ya
meno ambayo haipaswi kumezwa.
Kanuni
ya tatu ni kujizoeza njia nzuri za kupiga mswaki. Unapaswa kuushika
mswaki wako kwa namna ambayo visafishio (brashi) vyake vitalenga kwenye
makutano ya meno na ufizi.
Unachotakiwa
kufanya ni kusafisha meno yako kwa mwendo mfupi wa kwenda mbele na
nyuma, juu na chini. Kumbuka kusafisha nje, ndani na sehemu za
kutafunia. Halikadhalika usisahau kusafisha ulimi kwa kutumia mswaki
wakati ukipiga mswaki.
Ni
muhimu kuutunza mswaki katika hali ya usafi kila baada ya kuutumia.
Mara zote safisha mswaki wako kwa maji safi umalizapo kuutumia.
Unapouhifadhi, usimamishe ili ukauke mpaka utakapoutumia tena.
Kama
una miswaki kadhaa na yote unaitunza mahali pamoja, tenganisha huu
uliotumia sasa na hiyo mingine ili kuzuia maambukizi ya bakteria. Weka
mswaki wako mahali penye hewa ya kutosha vinginevyo huweza kuchochea
ukuaji wa bakteria na fangasi kwenye mswaki wako ambao wanaweza
kukusababishia maambukizi ya mgonjwa ya kinywa au mwili kwa ujumla.
Kanuni
ya tano na mwisho kwa leo ni kutambua wakati sahihi wa kubadilisha
mswaki wako. Mswaki hupoteza ubora wake kadri uutumiavyo hivyo kustahili
kubadilishwa. Kila mtengenezaji anapaswa kuandika mswaki unaoununua
unastahili kutumika kwa muda gani…ingawa hufanya hivyo ila wengi
hatuzingatii kusoma maelekezo yaliyomo. Lakini ipo kanuni ya jumla.
Unatakiwa kuhakikisha unatumia mswaki mpya kila baada ya miezi matatu
mpaka minne. Ni vyema kama utafanya hivyo chini ya muda huo au pale
utakapoona umeanza kuharibika.
Flosi
ni uzi maalumu uliotengenezwa ili kusafisha katikati ya meno ambamo
brashi za mswaki haziwezi kufika na kutekeleza lengo hilo. Hivyo,
kuflosi ni kusafisha maeneo yaliyo kati ya jino na jino ambayo hayawezi
kufikiwa na mswaki.
Kutokana
na ugumu wa kupiga mswaki maeneno ya kati jino na jino, inashauriwa
kusafisha mara moja kwa siku ili kuimarisha usafi kamili wa kinywa na
kujihakikishia siha njema.
Zipo
kanuni au taratibu za kuzingatia. Kwanza unashauriwa kukata uzi wa
kufanyia flosi wa kutosha. Kwa mtu mzima, inapendekezwa uwe na urefu
walau sentimita 45.
Kisha
zungusha sehemu kubwa ya uzi huo kwenye kidole cha kati cha mkono mmoja
na fanya vivyo hivyo kwenye kidole cha kati cha mkono mwingine.
Flosi
hufanywa taratibu. Unashauriwa kuelekeza na kuupitisha uzi kati ya meno
ukitumia na kusugua. Sugua meno na sio ufizi. Fanya hivyo kutoka jino
moja kwenda jingine kwa zamu.
Flosi
jino moja kwa wakati mmoja. Jiridhishe kwa ukamilifu ulioufanya kwenye
jino la kwanza kabla hujahamia la pili. Flosi taratibu kwa kusugua
kwenye jino kwa kwenda juu na kushuka chini.
Habari
njema ni kwamba hujachelewa kwani ukifanya kazi yako vizuri, haijalishi
umeanza lini kupiga mswaki au kuflosi matokeo ni sawasawa. Utakuwa na
afya njema na utajiamini popote utakapokuwa.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: