
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Kamanda wa Polisi mkoa wa Dar es salaam Simon Sirro, amesema kama
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, ana wasiwasi na Jeshi la
Polisi katika operesheni ya kutokomeza matumizi ya Shisha, achukue hatua
zaidi kwa sababu yeye ni kiongozi wao na ni mwenyekiti wa kamati ya
ulinzi na Usalama Mkoani Dar es salaam.
Akiongea leo asubuhi, Sirro
amedai wao kama jeshi la Polisi wanafanya kazi kwa mujibu wa Sheria na
Operesheni ya kutokomeza Shisha jijini inaendelea kama kawaida kilicho
baki ni Mwanasheria mkuu wa Serikali kuandaa mashtaka kwa Watuhumiwa.
“Watu wamekamatwa ni wengi, kimsingi kazi inafanyika, sasa huo ni
wasi wasi kama wasi wasi basi unabaki kuwa wasi wasi, kikubwa niseme
tunafanya kazi kwa mujibu wa sheria na kanuni, yeye ni mwenyekiti wangu
wa kamati ya ulinzi na usalama kwa hiyo ninaamini kama ana wasiwasi na
chombo chake najua atakuja kutuita na kutuambia nini cha kufanya.
“Lakini kama ana wasi wasi Zaidi yeye ni kiongozi wetu atajua
atachukua hatua gani dhidi ya sisi, kwa hiyo namuachia mkuu wangu wa
kazi yeye ndio atajua nini cha kufanya”
Akitolea ufafanuzi kama alipatiwa taarifa juu ya watu 10 waliotaka
kumpa ‘Mlungula’ Mkuu wa Mkoa ili kumziba ‘Mdomo’ kukemea matumizi ya
kilevi cha Shisha, Kamanda Siro alisema hawezi kulisemea lolote swala
hilo na amemtaka Mtangazaji wa Sun Rise Stanslaus Lambat amuulize Mh
Makonda taarifa aliipeleka wapi na si yeye.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: