MKUU wa Wilaya ya Malinyi mkoa wa Morogoro, Majura Kasika ameagiza posho iliyookolewa kutokana na kufutwa kwa safari ya maofisa watatu na madereva wawili wa wilaya hiyo kwenda kwenye kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka huu mkoani Simiyu, kuelekezwa katika kuongezea nguvu ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa na matundu sita ya vyoo.


Hatua ya viongozi hao kufuta safari hiyo, ilitokana na agizo la Rais John Magufuli aliyeagiza viongozi kutoka mikoa yote nchini, nje ya Simiyu, kutokwenda katika maadhimisho hayo na wale ambao walikuwa tayari wamechukua posho kuzirejesha mara moja.

Kasika alisema jana kuwa kutokana na agizo hilo la Rais, wilaya ya Ulanga iliweza kuokoa Sh 2, 580,000 ambazo sasa zitaelekezwa katika kuchangia ujenzi huo wa vyumba viwili vya madarasa na matundu ya vyoo katika Shule ya Msingi ya Kitongoji cha Lumbanga Kijiji cha Misegesege Kata ya Malinyi.

Akizungumza na wananchi wa kitongoji hicho cha Lumbanga, wakati akiendesha kazi ya uhamasishaji wa uchangiaji wa michango ya maendeleo kwa ajili ya kupata fedha za kuanza kufyatua matofali ya ujenzi huo, Mkuu huyo wa wilaya alisema fedha hizo zitaelekezwa mara moja katika mradi huo.

Uamuzi huo wa Mkuu wa Wilaya, uliungwa mkono na Mbunge wa Malinyi, Dk Haji Mponda ambaye aliahidi kuchangia Sh 500,000 katika mpango huo, huku wananchi wakiahidi kuchangia Sh 30,000 kwa kila kaya.
DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: