
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
LICHA ya timu yake kuwa kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Kocha Mkuu wa Simba, Mcameroon Joseph Omog, amesema hajafurahishwa na pointi alizonazo katika mechi tano alizocheza za ligi hiyo inayotoa mwakilishi wa nchi katika mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Simba ambayo inadhaminiwa na Kampuni ya Kubashiri Matokeo ya SportPesa, huku ikiwa mabingwa wa Kombe la FA, ina pointi 11 sawa na Azam FC na Mtibwa Sugar, na imepoteza pointi nne ambazo zilitokana na sare mbili walizopata dhidi ya Azam FC na Mbao FC.
Akizungumza na gazeti la nipashe, Omog, alisema anahitaji kuongoza ligi huku akiwa na tofauti ya pointi zaidi ya tano ili kujihakikishia kumaliza mzunguko wa kwanza akiwa kwenye nafasi hiyo muhimu inayowaniwa na timu 16 zinazoshiriki ligi hiyo.
Omog alisema mawazo na akili yake ni kuhakikisha wanashinda mechi zao zinazofuata.
"Tulipoteza pointi mbili tulipocheza na Azam na tulipokwenda Mwanza vile vile, haikuwa jambo jema, lakini ndiyo matokeo ya mpira yalivyo, tunahitaji kuhakikisha hatupotezi tena pointi licha ya kuwa mechi zote ni ngumu," alisema Omog.
Aliongeza kuwa jana asubuhi nyota wake wote walifanya mazoezi kwa ajili ya kujiandaa na mechi dhidi ya Mtibwa Sugar itakayofanyika Jumapili kwenye Uwanja wa Uhuru jijini.
"Mechi zote ni muhimu na tutaingia uwanjani kuendelea kusaka ushindi, tunaziheshimu klabu zote kwa sababu wote tunashiriki ligi moja, tunapoingia uwanjani tunakuwa kwenye hadhi moja, hapo ndipo heshima ya kila upande inatakiwa kuonekana katika kusaka matokeo mazuri," Omog aliongeza.
Alisema kwa kiwango kikubwa kila idara kwenye kikosi hicho imefanya kazi nzuri, lakini kama timu inahitaji kuona wanaongeza bidii katika mechi zote zinazofuata.
Baada ya mchezo huo wa Jumapili dhidi ya Mtibwa Sugar inayofundishwa na Kocha Zuberi Katwila, kikosi hicho kitaendelea kufanya mazoezi ya kuikaribisha timu mpya iliyopanda daraja ya Njombe Mji na Oktoba 28 watakuwa wageni wa Yanga, mechi zote zikifanyika kwenye Uwanja wa Uhuru.
Post A Comment: