
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Polisi Wilaya ya Arusha imepiga marufuku mikutano ya hadhara ya Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema kwa maelezo kuwa kutakuwa na ujio wa viongozi wa kitaifa jijini hapa.
Pia, kuzuiwa mikutano ya mbunge huyo wa Chadema kumeelezwa kuchangiwa na kuungua moto kwa nyumba za polisi kwa kuwa jeshi hilo limeelekeza nguvu kubwa huko.
Barua iliyoandikwa jana na Mkuu wa Polisi Wilaya ya Arusha, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, E.Tille kwenda wa Lema inaeleza kuwa mikutano yake iliyokuwa ifanyike jana na leo imesitishwa.
Kwa kuwa siku hizo zina mwingiliano na ratiba za shughuli za kiserikali za viongozi wa juu wa Serikali inayoishia Oktoba 4.
Pia amesema janga la moto katika kambi ya Polisi lililotokea juzi usiku limeleta madhara makubwa hivyo, nguvu kubwa itaelekewa huko.
“Unashauriwa kupanga mikutano yako tarehe yoyote kuanzia Oktoba 5, 2017 pia rejea mazungumzo yangu na wewe ofisini kwangu ya tarehe 29/09/2017,” inasomeka barua hiyo.
Hata hivyo, Lema amepinga polisi kuzuia mikutano yake akisema ni ukiukwaji wa sheria na haki za mbunge.
Alisema Sheria ya Bunge, Kifungu cha Nne, Fasili ya kwanza, kinazungumzia uhuru wa mbunge kufanya mikutano jimboni kwake na Kifungu cha 4(1) na (2) vinaelezea uhuru huo wa mbunge kufanya mikutano na pia ni ukiukwaji wa sheria kuzuia mikutano yake kwenye jimbo lake.
Alisema anaamini, kuzuiwa kwa mikutano yake ni njama kwa kuwa awali alipanga kuzungumza na wananchi wa Kata ya Kimandolu ambako diwani wao amejiuzulu na kisha wananchi wa Mjini Kati.
“Kwanza waliniita wakaniambia hali ya kisiasa si nzuri nisiende kufanya mkutano Kimandolu kwa kuwa wananchi wanaweza kuwa na hasira baada ya diwani kujiuzulu, mimi nikawaambia wasiwe na hofu lazima likafanye mkutano,” alisema.
Alidai kwamba polisi wanaamini atazungumzia sakata la kupigwa risasi Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na pia ziara ya Rais John Magufuli jijini Arusha hivi karibuni na kwamba anashauriana na wanasheria wake kuona kama akubali barua ya polisi au aendelee na mikutano yake.
Hii ni mara ya pili kwa Lema kuzuiwa kufanya mikutano. Agosti 25 alizuiwa ili kupisha mbio za Mwenge wa Uhuru na mitihani ya darasa la saba na alitii agizo hilo.
Post A Comment: