
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Msanii wa filamu maarufu duniani na raia wa Marekani, Cynthia Rothrock, maarufu Lady Dragon, ametua kutalii katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Cynthia aliyewahi kushinda tuzo tano za filamu duniani kupitia filamu zake za mapigano, amefikia katika hoteli ya Grumeti Serengeti inayomilikiwa na bilionea wa Marekani, Paul Tudor.
Msanii huyo ambaye ameigiza zaidi ya filamu 31, miongoni wa zilizompa umaarufu ni Lady Dragon Xtreme Fighter na Deadliest Art.
Tangu atue nchini juzi Agosti 26, picha zake zimesambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii duniani.
Hata hivyo, kama ilivyokuwa kwa mchezaji maarufu wa Uingereza, David Backham, safari ya Cynthia ni ya mapumziko binafsi.
Akizungumzia ujio wa msanii huyo mwenye mkanda mweusi katika mchezo wa karate, Meneja Uhusiano wa Tanapa, Pascal Shelutete, amesema umetokana na kazi kubwa ya Serikali, Tanapa na wadau wengine kuitangaza Serengeti.
Shelutete amesema wasanii wengine wengi wakubwa duniani wanatarajiwa kuingia nchini, kutalii kama ambavyo imetokea mwaka huu.
βMwaka huu umekuwa mzuri katika utalii nchini, tumepata watalii wengi maarufu duniani, wakiwemo wachezaji mpira, wasanii wa filamu na viongozi wa kisiasa,β amesema.
Post A Comment: