
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu ameripoti jana Kituo Kikuu cha Polisi na ametakiwa kuripoti tena Septemba 11.
Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Benedict Kitalika amesema mwanasiasa huyo alifika kituoni jana Agosti 28 mchana kama alivyotakiwa na jeshi hilo.
"Nimeongea na msaidizi wa ZCO (Mkuu wa Upelelezi Kanda) anasema ameripoti . Muda umesogezwa sana kwa sababu kuna majukumu mengine yanashughulikiwa kwa sasa," amesema Kitalika.
Lissu ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki, alikamatwa na polisi mwishoni mwa wiki iliyopita akiwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akituhumiwa kumkashifu Rais John Magufuli wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari kwenye hoteli ya Protea siku chache zilizopita.
Siku ya mkutano huo, Lissu aliibua sakata linalohusu kampuni ya Stirling Civil Engineering Ltd (SCEL) kushikilia ndege ya Bombardier Dash 8 nchini Canada hadi Serikali itakapoilipa deni la Sh87 bilioni.
Katika sakata hilo, Lissu alimhusisha Rais ambaye wakati huo alikuwa waziri wa ujenzi kwa kuvunja mkataba wa ujenzi wa Barabara ya Tegeta Wazo Hill -Bagamoyo iliyokuwa ikijengwa na SCEL.
Post A Comment: