
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
BEKI wa zamani, Jamie Carragher, ameingilia kati mvutano unaoendelea kati ya klabu yake ya zamani ya Liverpool na Barcelona juu ya nyota Philippe Coutinho.
Barca wameendelea kung’ang’ania mpango wao wa kumsajili Mbrazil huyo ingawa wameshaambiwa na mabosi wa Anfield kwamba hauzwi kwa kiasi chochote cha fedha.
Kwa upande wake, mkongwe Carragher, ambaye alikuwa kwenye kikosi cha Liver kilichotwaa taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya mwaka 2006, amesema kuuzwa kwa Coutinho si tatizo kama ambavyo ingekuwa kwa Sadio Mane.
Mkongwe huyo amedai kuwa Mane ana umuhimu mkubwa kikosini kuliko Coutinho.
“Najua nitatengeneza mjadala mkubwa kutokana na falsafa ya Jurgen Klopp, lakini nafikiri Mane ni muhimu zaidi kwenye kikosi cha Liverpool,” alisema Carragher.
Mane aliifungia Liver bao la ushindi dhidi ya Crystal Palace kwenye mchezo wa kwanza wa ufunguzi wa msimu huu uliochezwa kwenye Uwnaja wa Anfield, ambapo Coutinho aliukosa mtanange huo kutokana na maumivu ya mgongo.
Carragher anaamini Msenegal huyo ndiye aliyekuwa moto wa kuotea mbali msimu uliopita na kuisaidia Liver kumaliza nafasi ya nne kwenye msimamo wa Ligi Kuu England.
“Angalia anafunga mabao yake, jinsi yalivyo muhimu kwenye timu tangu alipojiunga na timu hiyo. Ni mchezaji wa pembeni sawa, lakini ana idadi kubwa ya mabao akikimbizana na washambuliaji,” alisema Carragher.
“Kama tutamlinganisha na Coutinho anayetakiwa na Barcelona, bado Mane ana sababu ya kutembea kifua mbele. Akiendelea kwa kasi ile na kiwango kile basi atazivutia timu kubwa zaidi barani Ulaya.”
Hata hivyo, Carragher anaamini kwamba, Coutinho hataondoka Liver licha ya Barca kumkalia kooni wakimtaka kuziba pengo la Neymar.
“Bado wataendelea kumng’ang’ania kwa sababu ni moja ya wachezaji muhimu kwenye klabu. Sioni kama ni vibaya kumbakiza kwa wakati huu,” alisema.
Post A Comment: