
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
.MCHAKAMCHAKA wa Ligi ya Mabingwa Ulaya unaendelea wiki huu ambapo vigogo Real Madrid, Barcelona na Manchester United watahakikisha wanapanga vikosi vya maana ili kupata tiketi yao ya kutinga hatua ya mtoano ya 16 bora.
Liverpool, Chelsea na Juventus nazo hazipo kwenye nafasi ngumu ya kupenya, lakini mashaka makubwa yapo Atletico Madrid, ambao wanaweza kuaga mapema tu michuano hiyo sawa na ilivyo kwa wakali wa Serie A msimu huu, Napoli.
Real Madrid inayoonekana kuwa kwenye ubora duni msimu huu, watahitaji kushinda ugenini kwa APOEL kujihakikishia nafasi, wakati wenzao kwenye kundi lao, vinara Tottenham Hotspur watakuwa na shughuli huko Ujerumani kuwavaa Borussia Dortmund.
Mechi hizo zote zinapigwa leo Jumanne, sambamba na Napoli watakaokuwa nyumbani kuwakaribisha Shakhtar Donetsk, Monaco watakipiga na RB Leipzig, Sevilla na Liverpool, Spartak Moscow na Maribor, Besiktas na Porto na Manchester City wao watakuwa Etihad kuwakaribisha Feyenoord.
Kesho, Jumatano, michuano hiyo itaendelea kwa Man United wakiwa ugenini kwa FC Basel huku huko Turin kukiwa na bonge la mechi kati ya Juventus na Barcelona.
Bayern Munich wakisafiri kuifuata Andetletch, PSG watakuwa nyumbani kuwakaribisha Celtic na Atletico Madrid watakipiga na AS Roma, huku Sporting CP watakuwa mwenyeji wa Olympiakos, Chelsea wakiwa ugenini kwa Qabarag na CSKA Moscow watakuwa kwao kucheza na Wareno Benfica.
Post A Comment: