Msanii wa muziki wa bongo fleva Alikiba ambaye amepewa cheo cha 'Mfalme' na mashabiki wake, amedhihirisha kuwa mashabiki hawakukosea kumpa cheo hicho, kwa kuvunja rekodi ya kutazamwa kwa video yake kwa mara nyingi zaidi ndani ya muda mfupi.


Kwenye ukurasa wake wa instagram, Alikiba ambaye siku ya Ijumaa ameachia video ya wimbo mpya ya 'Seduce me', ameweka post akiwashukuru mashabiki wake kwa kufanikisha kuvunja rekodi hiyo.

"Ahsanteni sana kwa upendo, nisingebarikiwa zaidi na kupendelewa bila nyinyi, nyinyi ni wa maana sana kwangu na nafanya haya kwa ajili yenu", aliandika Alikiba.

Pamoja na hayo kwenye ukurasa wa instagram wa kampuni kubwa inayosimamia muziki wa Alikiba ya Rockstar. imeandika kuhusu rekodi ya video hiyo ambayo bado inaendelea kushika namba moja kweny video zinazotrend.

Historia ya kuvunjwa rekodi imewekwa, Mfalme Kiba na wimbo wake mpya wa 'Seduce me' umekuwa wa kwanza na kipee kwa msanii wa Afrika Mashariki kufikia kutazamwa mara milioni 1 kwenye Vevo/YouTube ndani ya masaa 38 tu, ina 'trend'namba 1 Tanzania na namba 1 Kenya kwa 'weekend' nzima, rekodi imevunjwa”, iliandika Rockstar.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: