
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Beki mpya wa Simba, Erasto Nyoni ameanza kufuata nyayo za beki mwingine wa timu hiyo, Shomari Kapombe katika kutupia mabao.
Kapombe ndiye beki alifunga mabao mengi katika miaka ya karibuni ambapo alifunga mabao manane Ligi Kuu msimu wa 2015/16.
Hata hivyo Nyoni ambaye ametua Simba msimu huu, ameanza kuweka rekodi ya aina yake baada ya kufunga mabao manne katika mechi nane alizocheza hivi karibuni.
Nyoni alianza kwa kufunga bao safi kwenye mchezo wa Taifa Stars na Zambia katika michuano ya COSAFA kabla ya kufunga tena katika mchezo wa kirafiki kati ya Bidvest Wits ya Afrika Kusini na Simba.
Beki huyo anayemudu kucheza nafasi zote za ulinzi, alifunga pia dhidi ya Gulioni ya Zanzibar kabla ya kufunga tena dhidi ya Ruvu Shooting juzi Jumamosi hivyo kuwa beki wa Simba aliyecheka na nyavu zaidi.
Post A Comment: