
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 24 Desemba, 2016 amewasili
mkoani Singida na kupokelewa na mkuu wa Mkoa wa huo Dkt. Rehema
Nchimbi na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Singida.
Rais Magufuli na Mkewe Mama Janeth
Magufuli, kesho tarehe 25 Desemba 2016 wanatarajia kuungana na waumini
wengine wa dini ya Kikristo nchini katika ibada ya Sikukuu ya Krismasi
mkoani Singida.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa
Singida Dkt. Rehema Nchimbi amewaomba waumini wa dini ya kikristo mkoani
Singida kujitokeza kwa wingi kuungana na Rais Magufuli katika ibada ya
Krismasi kwani imekuwa ni heshima kwao kutokana na uwepo wa Rais
Mkoani hapa kwa ajili ya sikukuu ya Krimass.
Dkt. Nchimbi amewataka wananchi wa
mkoa wa Singida na Tanzania kwa ujumla kuendelea kumuombea Rais
Magufuli na familia yake ili aendelee kuwatumikia watanzania katika
kuwaletea maendeleo.
Amesema ni bahati kubwa kwa mkoa
wa Singida kwa mara nyingine tena kumpokea Kiongozi huyo Mkuu wa nchi
kwa kuwa katika kipindi kifupi mkoa huo pia ulimpokea Waziri Mkuu wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa alipohudhuria
sherehe za Maulidi.
Jaffar Haniu
Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Singida
24 Desemba, 2016
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: