
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Rais John Magufuli ameomboleza kifo cha mkuu wa mkoa mstaafu, Joel Bendera kilichotokea katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).
βJioni hii nimepokea kwa mshtuko na huzuni kubwa taarifa za kifo cha Mkuu wa Mkoa mstaafu Dk Joel Nkaya Bendera, natoa pole kwa familia yake na wote walioguswa na msiba huu, pia naungana nao katika kipindi hiki cha majonzi,β amesema Rais Magufuli katika taarifa iliyotolewa na Ikulu leo Jumatano Desemba 6,2017.
Bendera amefariki dunia jioni ya leo katika Hospitali ya Muhimbili alikofikishwa kwa ajili ya kupata matibabu.
Rais Magufuli amesema Bendera atakumbukwa kwa mchango alioutoa kwa Taifa akiwa kiongozi katika nyadhifa mbalimbali zikiwemo ukuu wa mkoa, naibu waziri na mbunge. Pia, katika maendeleo ya michezo.
βAlikuwa kiongozi shupavu, mahiri na mchapakazi, alipenda kufanya kazi kwa ushirikiano na daima alitamani kupata mafanikio makubwa katika majukumu aliyokuwa nayo, hakika tutamkumbuka,β amesema Rais Magufuli.
Pia, amewapa pole wananchi wa mikoa ya Manyara alikokuwa mkuu wa mkoa Oktoba 26,2017 na mkoani Tanga alikokuwa mbunge.
Rais Magufuli ametoa pole kwa wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM), wanamichezo na wote walioguswa na msiba huo.
Post A Comment: