
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul
Makonda, amewaagiza wakuu wa wilaya mkoani mwake, kutokubali kubomolea nyumba
wananchi bila kujiridhisha kwa hukumu halali za Mahakama.
Pia Jeshi la Polisi limetakiwa kutosimamia
mchakato wa ubomoaji nyumba bila Mkuu wa Wilaya kujiridhisha na uhalali wa
kubomoa.
Makonda alisema hayo jana wakati akimwapisha
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Kisare Makori aliyechukua nafasi ya Humphrey Polepole
aliyeteuliwa kuwa Katibu Mwenezi wa CCM.
Alisema kuna tabia mkoani humo ya watu
kutekeleza hukumu za Mahakama na zingine zikiwa feki kwa kubomolea wananchi
nyumba zao.
“Hakuna mtu anayeruhusiwa kubomoa nyumba
bila ninyi (wakuu) kujiridhisha kwamba ana hukumu halali ya Mahakama, kama hana
hukumu halali una nafasi ya kuchukua hatua,” alisema huku akibainisha kutumia
wanasheria wa mkoa na manispaa hizo kupitia nyaraka zote.
”Kwa hiyo wale wote sijui Majembe Auction
… hawaruhusiwi kubomoa nyumba hadi DC uwe na uhakika kwamba hatua za hukumu
zimepitishwa kihalali,” alisema.
Alisema kufanya hivyo kutasaidia kuzuia
kilio cha wanyonge na masikini ambao wanabomolewa nyumba na baada ya siku
inagundulika kuwa hukumu ni bandia.
“Nawaagiza wakuu wa wilaya simamieni
hilo, ili mwakani tuongeze kasi ya kutetea wanyonge. Hakuna mtu mwenye mamlaka
ya kubomoa nyumba kama wewe hujaridhika,” alisema.
Makonda aliitaka Polisi kutoshiriki
mchakato wa kuvunja nyumba za wananchi hadi DC atakapojiridhisha.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: