MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, amewaagiza wakuu wa wilaya mkoani mwake, kutokubali kubomolea nyumba wananchi bila kujiridhisha kwa hukumu halali za Mahakama.

Pia Jeshi la Polisi limetakiwa kutosimamia mchakato wa ubomoaji nyumba bila Mkuu wa Wilaya kujiridhisha na uhalali wa kubomoa.

Makonda alisema hayo jana wakati akimwapisha Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Kisare Makori aliyechukua nafasi ya Humphrey Polepole aliyeteuliwa kuwa Katibu Mwenezi wa CCM.

Alisema kuna tabia mkoani humo ya watu kutekeleza hukumu za Mahakama na zingine zikiwa feki kwa kubomolea wananchi nyumba zao.

“Hakuna mtu anayeruhusiwa kubomoa nyumba bila ninyi (wakuu) kujiridhisha kwamba ana hukumu halali ya Mahakama, kama hana hukumu halali una nafasi ya kuchukua hatua,” alisema huku akibainisha kutumia wanasheria wa mkoa na manispaa hizo kupitia nyaraka zote.

”Kwa hiyo wale wote sijui Majembe Auction … hawaruhusiwi kubomoa nyumba hadi DC uwe na uhakika kwamba hatua za hukumu zimepitishwa kihalali,” alisema.

Alisema kufanya hivyo kutasaidia kuzuia kilio cha wanyonge na masikini ambao wanabomolewa nyumba na baada ya siku inagundulika kuwa hukumu ni bandia.

“Nawaagiza wakuu wa wilaya simamieni hilo, ili mwakani tuongeze kasi ya kutetea wanyonge. Hakuna mtu mwenye mamlaka ya kubomoa nyumba kama wewe hujaridhika,” alisema.

Makonda aliitaka Polisi kutoshiriki mchakato wa kuvunja nyumba za wananchi hadi DC atakapojiridhisha.  

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: