MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, imefuta kesi ya kupokea rushwa ya Sh milioni 161.7 iliyokuwa ikimkabili aliyekuwa Mhandisi Mkuu wa Wakala wa Umeme Vijijini (REA), Theophillo Bwakea.


Bwakea aliyedaiwa kupokea fedha hizo kutoka kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya VIP Engineering, James Rugemalila ambazo ni sehemu ya fedha zilizokuwamo kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow.

Wakili wa Serikali, Odesa Olombe alidai jana mbele ya Hakimu Mkazi, Respicius Mwijage kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika na kwamba wanaomba mahakama ifute kesi hiyo.

Olombe alidai kuwa wanaomba kufuta kesi hiyo kwa mujibu wa kifungu namba 98 (a) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai kifungu kidogo cha 25 kilichofanyiwa marekebisho mwaka 2002. Kutokana na maombi hayo, wakili wa mshitakiwa Rweyongeza Richard, alidai kuwa hana pingamizi na maombi ya upande wa Jamhuri.

Hata hivyo, Hakimu Mwijage alikubaliana na ombi lililotolewa na upande wa jamhuri na kuifuta kesi hiyo. Inadaiwa kwamba kabla ya Bwakea kufanya kazi REA, alikuwa Wizara ya Nishati na Madini, kitengo cha kusimamia umeme, ambako anadaiwa alishiriki kutunga sera ya kampuni binafsi kuuza umeme Shirika la Umeme (Tanesco).

Inaelezwa kuwa sera hiyo ilipoanza kutumika, Kampuni ya Kufua Umeme ya IPTL ilikuwa ya kwanza kupata zabuni. Inadaiwa Februari 12, 2014 katika Benki ya Mkombozi, mshitakiwa akiwa Mhandisi Mkuu wa REA, kwa njia ya rushwa alijipatia Sh milioni 161.7 kupitia akaunti namba 00410102643901 fedha ambazo ni sehemu ya zilizokuwapo katika Akaunti ya Tegeta Escrow.

Pia inadaiwa fedha hizo aliingiziwa katika akaunti yake na Rugemalila ambaye ni mshauri binafsi wa kimataifa, Mkurugenzi wa VIP Engineering na alikuwa Mkurugenzi wa IPTL. Hata hivyo, inadaiwa alipewa fedha hizo kama zawadi kwa kuwa alikuwa mmoja wa wajumbe walioandaa sera zilizoruhusu sekta binafsi kuuza umeme Tanesco.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: