
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, imefuta kesi ya kupokea rushwa ya Sh
milioni 161.7 iliyokuwa ikimkabili aliyekuwa Mhandisi Mkuu wa Wakala wa
Umeme Vijijini (REA), Theophillo Bwakea.
Bwakea aliyedaiwa kupokea fedha hizo kutoka kwa Mkurugenzi wa Kampuni
ya VIP Engineering, James Rugemalila ambazo ni sehemu ya fedha
zilizokuwamo kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow.
Wakili wa Serikali, Odesa Olombe alidai jana mbele ya Hakimu Mkazi,
Respicius Mwijage kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika na kwamba
wanaomba mahakama ifute kesi hiyo.
Olombe alidai kuwa wanaomba kufuta kesi hiyo kwa mujibu wa kifungu
namba 98 (a) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai kifungu kidogo
cha 25 kilichofanyiwa marekebisho mwaka 2002. Kutokana na maombi hayo,
wakili wa mshitakiwa Rweyongeza Richard, alidai kuwa hana pingamizi na
maombi ya upande wa Jamhuri.
Hata hivyo, Hakimu Mwijage alikubaliana na ombi lililotolewa na
upande wa jamhuri na kuifuta kesi hiyo. Inadaiwa kwamba kabla ya Bwakea
kufanya kazi REA, alikuwa Wizara ya Nishati na Madini, kitengo cha
kusimamia umeme, ambako anadaiwa alishiriki kutunga sera ya kampuni
binafsi kuuza umeme Shirika la Umeme (Tanesco).
Inaelezwa kuwa sera hiyo ilipoanza kutumika, Kampuni ya Kufua Umeme
ya IPTL ilikuwa ya kwanza kupata zabuni. Inadaiwa Februari 12, 2014
katika Benki ya Mkombozi, mshitakiwa akiwa Mhandisi Mkuu wa REA, kwa
njia ya rushwa alijipatia Sh milioni 161.7 kupitia akaunti namba
00410102643901 fedha ambazo ni sehemu ya zilizokuwapo katika Akaunti ya
Tegeta Escrow.
Pia inadaiwa fedha hizo aliingiziwa katika akaunti yake na Rugemalila
ambaye ni mshauri binafsi wa kimataifa, Mkurugenzi wa VIP Engineering
na alikuwa Mkurugenzi wa IPTL. Hata hivyo, inadaiwa alipewa fedha hizo
kama zawadi kwa kuwa alikuwa mmoja wa wajumbe walioandaa sera
zilizoruhusu sekta binafsi kuuza umeme Tanesco.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: