
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
BEKI wa pembeni wa klabu ya Simba, Mohamed
Hussein 'Tshabalala' amefunguka juu ya hatma yake ndani ya kikosi hicho
akisisitiza bado ni mali ya halali ya timu hiyo.
Akizungumza jana, Tshabalala, alisema mkataba wake na
klabu hiyo umebakia miezi sita, lakini anaipa heshima timu hiyo
linapokuja suala la hatma yake.
Kauli ya mchezaji huyo inapingana na ile ya uongozi wa juu wa timu
hiyo ambao walikaririwa wakisema nyota huyo bado ana mkataba wa mwaka
mmoja.
"Kwa sasa nimepumzika na nisingependa kuongea sana kuhusu hayo mambo,
ila mimi bado mali ya Simba japo mkataba wangu umebakiza miezi sita
kumalizika," alisema Tshabalala.
Aidha, alipoulizwa kama ameanza mazungumzo na klabu hiyo kwa ajili ya
mkataba mpya, Tshabalala, alisema jambo hilo linashughulikiwa na meneja
wake.
"Mambo yakiwa tayari mtafahamu tu, lakini kuhusu mkataba mpya au kitu
kingine, meneja wangu anafuatilia, tuwe na subira," alisema beki huyo
wa pembeni ambaye pia anachezea timu ya Taifa 'Taifa Stars'.
Tshabalala, alisema yeye ni mchezaji na siku zote mpira ndio maisha
yake, hivyo ni makini kwa kila jambo linapokuja suala la usajili au
kupata mkataba mpya.
Juzi katibu Mkuu wa Simba, Patrick Kahemele, alisema timu hiyo ipo
kwenye mazungumzo na Tshabalala kwa ajili kumuongezea mkataba mpya.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: