Klabu ya Arsenal ipo katika hatua nzuri ya kukamilisha mpango wa kuwasainisha mikataba mipya wachezaji wake Alexis Sanchez na Mesut Ozil chini ya ushawishi mkubwa unaoendelea kufanywa na meneja Arsene Wenger.


Taarifa zinasema kuwa, Wenger amependekeza wawili hao wasainishwe mkataba wa miaka miwili, ambayo itakua chachu ya kuanza kulipwa mishahara minono kutokana na kazi nzuri na kubwa wanayoifanya kwa ajili ya maendeleo ya Arsenal tangu walipotua klabuni hapo.

Mwishoni mwa juma lililopita Wenger aliwaeleza waandishi wa habari “Tupo tayari kuvunja benki kwa ajili ya kukamilisha mpango wa kusainiwa kwa mkataba mpya wa Ozil ambao utamuwezesha kupokea mshahara wa Pauni 250,000 kwa juma.”

Hali kadhali kauli kama hiyo aliitoa alipoulizwa kuhusu maendeleo ya mazungumzo kati ya uongozi wa Arsenal na Sanchez.

Wenger kwa sasa anamalizia muda wa mwaka mmoja uliosalia kwenye mkataba wake, lakini amekua na matumaini makubwa ya kuwabakisha wachezaji hao klabuni hapo kwa ajili ya maslahi ya baadae.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI

ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: