
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
BARAZA la Mitihani Tanzania (Necta) limeunda mfumo wa kutunza taarifa
za wanafunzi wa Shule za Msingi (PReM), ambao utasaidia katika
uandikishaji wa wanafunzi wote na kupewa namba maalumu, ambayo
itamtambulisha mwanafunzi katika ngazi mbalimbali za mafunzo na hivyo
kuondoa tatizo la wanafunzi hewa.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, jijini Dar es Salaam kuhusu
mafanikio ya baraza hilo, Ofisa Habari wa Necta, John Nchimbi alisema
mfumo huo pia utasaidia katika uhamisho wa mwanafunzi kutoka shule moja
hadi nyingine ndani ya mkoa au nje ya mkoa.
Alisema mfumo huo utarahisisha utaratibu unaotumika sasa wa kuhamisha
mwanafunzi kutoka shule moja hadi nyingine na kuweza kuondoa tatizo la
wanafunzi hewa na pia utasaidia katika uandaaji na utoaji wa takwimu za
wanafunzi katika ngazi ya shule, wilaya, mkoa hadi ngazi ya Kitaifa.
Aidha, alisema mfumo huo utasaidia katika ufuatiliaji wa taarifa za
matokeo ya kila mwanafunzi ili kuhakikisha wadau mbalimbali wa elimu
wanapata ufahamu wa kutosha kuhusu ufundishaji na ujifunzaji katika
ngazi ya shule.
Alisema baraza limeanza kufanya majaribio ya mfumo huo katika mikoa
miwili ya Mwanza na Ruvuma na ifikapo Desemba mfumo huo utaimarishwa ili
Januari hadi Mei mwaka 2017, utumiwe na mikoa yote kusajili wanafunzi
wa shule za msingi.
“Mfumo huu utadhibiti sana udanganyifu kwa sababu kila mwanafunzi
anapoanza shule atapatiwa namba ambayo ataendelea nayo hiyo hiyo katika
elimu ya sekondari kidato cha nne hadi cha sita…mfumo huu utakuwa na
picha hivyo kudhibiti udanganyifu,” alisema.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA
ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
Post A Comment: