Chama cha Wananchi (CUF), kimeendelea kudai kuwa mgombea wake wa urais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharrif Hamad alishinda na kunyang’anywa ushindi katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana.


Akizungumza mjini hapa jana, Maalim Seif ambaye pia ni katibu mkuu wa chama hicho, amesema hakuna namna yoyote watawala wataweza kuzuia haki ya uamuzi wa Wazanzibari walioutoa Oktoba 25, 2015, lakini kinachoendelea ni njama za kuichelewesha.

Maalim amesema hayo wakati akitoa salamu kwa waumini wa Dini ya Kiislamu waliofika kwenye ibada ya Ijumaa katika Msikiti wa Biziredi.

CUF wanalalamikia ushindi huo zikiwa zimepita siku 215 tangu uchaguzi wa marudio ulipofanyika Zanzibar.
DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: