TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI ​

Taarifa inatolewa kwa vyombo vya habari kuwa Kamati Kuu ya Chama itakutana kwa siku mbili, kuanzia Oktoba 22-23, mwaka huu, katika kikao chake cha kawaida.

Kikao hicho kitakachofanyika jijini Dar es Salaam, pamoja na agenda mbalimbali, kitapokea na kujadili kwa kina taarifa ya hali ya siasa nchini na mwelekeo wa nchi kwa ujumla kiuchumi na kijamii.

Aidha, Kamati Kuu pia itapokea na kujadili taarifa ya fedha na Mpango wa Uchaguzi wa Kanda 10 za Chama, kabla ya Sekretarieti kuanza utekelezaji, ambao utahusisha kuwa na shughuli za chama, kisiasa na kiutendaji, ikiwa ni pamoja na kuendelea kuwatumikia wananchi, operesheni za uimarishaji wa chama nchi nzima na kuendelea kutoa elimu ya uraia.

Imetolewa leo Ijumaa, Oktoba 21, 2016 na;

Tumaini Makene Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano CHADEMA
 
DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: