
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
KLABU ya soka ya Mtibwa Sugar haina mpango na usajili wa dirisha dogo linaloendelea kwa timu za Ligi Kuu Tanzania Bara, kutokana na kocha wao, Zuberi Katwila, kuweka wazi kuwa hahitaji kuongeza wachezaji wapya.
Akizungumza na gazeti la BINGWA, Katwila alisema ana kikosi kipana ambacho kimeimarika kila idara ndio maana hafikirii kufanya usajili katika dirisha dogo.
Alieleza kuwa anaweza kusajili iwapo baadhi ya wachezaji waliopo sasa wataondoka na kuacha pengo katika kikosi hicho.
βSina matarajio ya kusajili kwa sababu nawaamini wachezaji waliopo kwani wengi ni vijana na baadhi yao bado hawajapata nafasi ya kucheza,β alisema Katwila.
Wachezaji waliosajiliwa katika dirisha kubwa lililofungwa Agosti 6, mwaka huu ni Hassan Isihaka kutoka African Lyon, Hassan Dilunga (JKT Ruvu) na Kelvin Sabato (Majimaji).
Kikosi cha Mtibwa kinashika nafasi ya tano katika msimamo wa ligi kuu, baada ya kufikisha pointi 18 huku Simba wakiwa kileleni kwa idadi ya mabao mengi, lakini wakiwa na pointi 23 sawa na Azam.
Post A Comment: