
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Mshambuliaji mkongwe wa Majimaji, Danny Mrwanda amejiunga kwa mkopo na timu ya JKT Mlale.
Mrwanda aliyewahi kutamba akiwa Simba na Yanga na katika klabu mbalimbali za barani Asia alipokuwa akicheza soka la kulipwa amejiunga na JKT Mlale inayoshiriki ligi daraja la kwanza kwa mkopo wa mwaka mmoja.
Taarifa iliyotolewa na Uongozi wa Klabu hiyo kupitia kwa Ofisa Habari wake, Onesmo Ndunguru ilisema mshambuliaji huyo ameridhia kutua katika timu hiyo bila kinyongo chochote.
Ndunguru alisema kuwa kutokana na changamoto za kukosa namba uwanjani wameona ni bora akaitumikie JKT Mlale kuliko kukaa benchi na kupungua kiwango chake.
“Bado tuna mkataba nae wa mwaka mmoja ambao huo mkataba atakwenda kuumalizia huko Mlale ambako uongozi umempeleka kwa ajili ya kumfanya aendelee kuonyesha uwezo wake na timu hiyo ya daraja la kwanza,’’alisema Ndunguru
Mrwanda alisema kutua kwake JKT Mlale siyo kwamba ameshuka kiwango bali ni timu kama zilivyo za Ligi Kuu Tanzania Bara.
Alisema ‘Ninaimani ninakwenda kuonyesha kipaji kama nilivyofanya kwa timu zingine za Bara ninaiona ni timu nzuri na kwa ushirikiano pamoja na kujituma tutaivusha JKT Mlale kwenda Ligi Kuu.”
Kuhusu usajili wa wachezaji wapya katika kipindi hiki cha dirisha dogo linalotarajia kufungwa Disemba 15 mwaka huu,Ndunguru alisema uongozi hadi sasa haujaweka wazi ni wachezaji wangapi watasajili na nafasi zao.
“Kufanya usajili siyo lazima kwani kikosi ni kikubwa, kocha Habib kondo akiwanoa vyema wanaweza kuisaidia timu kumaliza ligi katika nafasi nzuri zaidi kuliko kujaza wachezaji halafu matunda yasionekanae.”
Post A Comment: