
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
MFANYAKAZI wa Mgodi wa Geita (GGM), Milembe Suleiman, anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Geita kutokana na kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja.
Awali, picha za video za mtuhumiwa huyo zilisambaa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii , zikimuonyesha akiwa na anayedaiwa kuwa mpenzi wake katika tukio linaloelezewa kuwa ni la kuvishana pete ya uchumba baina ya wawili hao.
Mijadala mbalimbali ya kuwalaani wawili hao ilipamba moto kwenye mitandao ya kijamii, hasa facebook na kwenye makundi mbalimbali ya whatsapp, binti mrembo anayedaiwa kuwa ndiye mke mtarajiwa wa mtuhumiwa akidaiwa kuwa ndugu wa mmoja wa naibu mawaziri wa serikali ya sasa ya awamu ya tano.
Wawili hao wanaonekana kwenye picha za video wakikumbatiana, kubusiana, kunyonyana ndimi kama wapenzi na pia ‘biharusi’ mtarajiwa akionyesha kwa madaha kidole chake chenye pete huku wakishangiliwa mara kadhaa na watu waliokuwa nao kwenye eneo la tukio lililokuwa na meza iliyojaa vinywaji na ‘makulaji’.
Hata hivyo, Nipashe haikupata uthibitisho kutoka kwenye chanzo huru kuhusiana na ukweli juu ya uhusiano wa binti huyo na naibu waziri.
Akizungumza na Nipashe jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Mponjoli Mwabulambo, alisema kuwa wanamshikilia Milembe , ambaye ni Ofisa Ugavi Kitengo cha Manunuzi wa GGM, kwa uchunguzi kabla ya kuchukuliwa kwa hatua zaidi za kisheria kwakuwa vitendo vya mapenzi ya jinsia moja haviruhusiwi nchini.
Alipoulizwa juu ya suala hilo jana, Makamu wa Rais wa GGM anayeshughulikia uendeshaji, Simon Shayo, alikiri kuwa Milembe ni mfanyakazi wa mgodi huo.
Hata hivyo, Shayo alisema kwakuwa jambo hilo linashughulikiwa na polisi, hawawezi kulizungumzia kwa sasa.
“Amekamatwa kwa makosa hayo. Tunasubiri polisi wafanye kazi zao… hatuwezi kuingilia kwa sababu makosa hayo hakuyatenda akiwa kazini. Alikuwa uraiani, kampuni haihusiki na vitendo vya mtu akiwa mtaani,” alisema Shayo.
Post A Comment: