
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Klabu ya Simba SC imethibitisha kuwa Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe atakuwa mgeni rasmi kwenye mkutano mkuu wa klabu hiyo unafanyika leo.
Mkutano huo mkuu maalum wa klabu utakuwa na lengo moja tu ambalo ni kumtangaza mzabuni aliyeshinda kumliki sehemu ya klabu kupitia mfumo wa hisa ambao utaanza kutumika kuendesha klabu hiyo.
Taarifa iliyotolewa jana na klabu hiyo imeeleza kuwa, βKwenye mkutano huu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe anatarajiwa kuwa mgeni rasmiβ.
Simba tayari imeshapitia hatua mbalimbali za ubadilishaji wa uendeshaji na umiliki wa klabu ambapo serikali na shirikisho la soka nchini TFF vimebariki mabadiliko hayo kwa manufaa ya maendeleo ya soka nchini.
Mkutano huo maalum utafanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam na historia itaandikwa kwa mara ya kwanza katika soka la Tanzania.
Post A Comment: