
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
SIMBA sasa washindwe wenyewe iwapo wanahitaji huduma ya mshambuliaji wa Nkana FC ya Zambia, Walter Bwalya, baada ya mchezaji huyo kuweka wazi kuwa yupo tayari kutua Msimbazi iwapo pande hizo mbili zitafikia makubaliano.
Benchi la ufundi la Simba linaloongozwa na Mcameroon Joseph Omog, wamependekeza kutafutiwa mshambuliaji mwenye uwezo wa hali ya juu, huku wakilitaja jina la Bwalya na tayari jukumu la kumfikisha mshambuliaji huyo Msimbazi, ametwishwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya klabu hiyo, Zacharia Hans Poppe.
Kigogo mmoja mwenye ushawishi mkubwa ndani ya Simba, ameliambia gazeti la BINGWA kuwa dau la Bwalya litakuwa kubwa, lakini Kamati ya Usajili chini ya Poppe itafanya kila linalowezekana wazungumze naye kwani wana uwezo wa kujichangisha kupata fedha atakazozihitaji.
βUnajua yule jamaa (Bwalya) kama unakumbuka misimu kadhaa, tulitaka kumsajili, lakini dau lake likawa kubwa sana, tukamshindwa lakini sasa tumeona tufanye kila linalowezekana tumchukue,β alisema.
Wakati Simba wakiendelea na mchakato huo, tayari mmoja wa viongozi wa Azam anatarajia kutua Zambia kumalizana na mchezaji huyo ili kuja kuziba pengo la mshambuliaji wao wa zamani, Kipre Tchetche.
Azam wanaonekana kupania kumnasa Bwalya kwani ni miongoni mwa mapendekezo ya kocha wao, Aristica Cioaba, wakiwa wamelenga kukiboresha kikosi chao kiweze kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara unaowaniwa pia na mabingwa watetezi, Yanga pamoja na Simba.
βSi Simba pekee, niko tayari kucheza timu yoyote ile itakayokuja na ofa nzuri na kuridhika nayo,β alisema Bwalya.
Bwalya ambaye uraia wake una utata kutokana na kudaiwa kuwa ni Mkongo, huku pia akihusishwa na uraia wa Zambia, ni mmoja wa mastraika wenye uwezo mkubwa wa kucheka na nyavu na kama timu mojawapo kati ya Simba au Azam itafanikiwa kuinasa saini yake, itakuwa imelamba dume.
Post A Comment: